• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 9:50 AM
Wanahabari wavamiwa kwenye kesi ya aliyebaka mtoto wa waziri

Wanahabari wavamiwa kwenye kesi ya aliyebaka mtoto wa waziri

Na MAGDALENE WANJA

BARAZA la Wanahabari nchini (MCK) limetoa onyo kwa wanaowavamia wanahabari wakiwa kazini kuwa watakabiliwa na sheria.

Hii ni baada ya wanahabari wawili kupata majeraha Alhamisi walipovamiwa katika mahakama ya Nakuru wakati wa kusikizwa kwa kesi ya mshukiwa wa ubakaji ya mtoto wa waziri serikalini.

Mkurugenzi mkuu wa MCK David Omwoyo aliyezungumza na wanahabari baada ya kupiga ripoti kuhusu kisa hicho na maafisa wa polisi katika kituo ca Central mjini Nakuru alilaani kitendo hicho  akisema kuwa ni kinyume na haki za wanahabari.

Mkurugenzi mkuu wa MCK Bw David Omwoyo aungana na wanahabari kukemea uvamizi dhidi ya vyombo vya habari katika kituo cha polisi cha Central mjini Nakuru Desemba 27, 2018. Picha/ Magdalene Wanja

“Yeyote atakayewavamia wanahabari wakiwa kazini atachukuliwa hatua kali za kisheria kwani hiyo ni kukiuka haki za vyombo vya habari na zile za kibinafsi,” alisema Bw Omwoyo.

 Baadhi ya waliojeruhiwa ni mwanahabari wa KTN  Peter Kimani,  na mwenzake wa Mount Kenya Tv Eliud Mwangi.

Bw Kimani alisema kuwa kutokana na shambulio hilo, alipata majeraha katika sehemu zake za siri.

Bw Omwoyo alisema kuwa baadhi ya kaunti ambazo zimerekodi visa vingi vya mashambulizi dhidi ya wanahabari ni pamoja na Kilifi, Bungoma, Tharaka Nithi, Murang’a, Embu, Mombasa na Nairobi.

Aliongeza kuwa ofisi ya Mashtaka ya Umma pamoja na ile ya Huduma za Polisi imehakikishia MCK kwamba visa vyote vilivyoripotiwa vitashughulikiwa.

You can share this post!

SHANGAZI AKUJIBU: Nilimuacha nilipomfumania akiwa na dadangu

Hatuna nia ya kutwaa bandari ya Mombasa, China sasa yasema

adminleo