Kimataifa

Ghana yakataa dili nono ya Amerika kutokana na hitaji la kufichua data za raia

Na REUTERS April 28th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

ACCRA, Ghana:

GHANA jana ilikataa mkataba wa kuimarisha sekta yake ya afya na Amerika, ikisema iligundua makubaliano hayo yangesababisha itoe maelezo muhimu ya data.

Utawala wa Rais John Dramani Mahama ulikataa mpango ambapo uliihitaji kupata msaada wa kifedha kwa kuipa Amerika data yake muhimu ya kiafya.

Suala hilo hilo lilizima mazungumzo kati ya Amerika na Zimbabwe na pia mahakama ya Kenya ilizima mkataba kama huo baada ya kesi kuwasilishwa na Shirika moja la kiraia.

Msemaji wa serikali ya kigeni ya Ghana na serikali haikujibu jumbe za Reuters kuhusu suala hilo. Amerika nayo ilisema kuwa huwa haifichui maelezo kuhusu mikataba yake ya kibiashara na mataifa mengine.

“Tunaendelea kuangalia njia ya kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili,” msemaji wa serikali akasema.

Mnamo Septemba, utawala wa Amerika ulitangaza mbinu mpya ya kiulimwengu ambayo ni ya kuhakikisha mataifa maskini yanatelekeza wajibu katika kupambana na ukimwi, malaria, pumu, polio nchini mwao.

Hii ilikuwa mbinu ya kuyazuia mataifa hayo kutegemea msaada wa Amerika na kujitegemea.

Mamlaka ya Kimataifa ya Maendeleo Amerika ilivunjwa mapema mwaka huu.

Amerika ilikuwa imetuma Sh28.3 milioni kama msaada kwa Ghana ikiwemo Sh12.4 bilioni kwa sekta ya afya 2024, kabla ya Rais Donald Trump kuyapunguza msaada kwa nchi za kigeni.