• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:55 AM
Rais wa China akaangwa kwa nia yake ya kusalia madarakani milele

Rais wa China akaangwa kwa nia yake ya kusalia madarakani milele

Na AFP

BEIJING, CHINA

MPANGO wa Rais wa China Xi Jinping kutaka kuwa kiongozi wa maisha umewakera, na kuwashangaza watu wengi nchini humo.

Mmoja wao ni mhariri wa gazeti linalomilikiwa na serikali Bw Li Datong ambaye juzi alitumia maneno makali, ya lugha moja ya kigeni, mbele ya halaiki akilaani njama hiyo ya chama tawala cha Kikomunisti, Communist Party.

Chama hicho kinadai kuwa “umma unaunga mkono” mswada wa sheria unaopania kubatilisha kipengee cha Katiba kinachodhibiti mihula ambayo rais anapaswa kuhudumu.

Bunge la nchini hiyo, linalodhibitiwa na chama hicho tawala, linatarajiwa kupitisha mswada huo Jumapili.

Li ni miongoni mwa raia ambao wamekaidi amri ya serikali na kulalamika hadharani kuhusu mswada huo.

“Nilishangazwa na tangazo hilo. Sikuamini kwamba Rais Xi na chama chake wangechukua hatua hiyo. Inasikitisha zaidi,” Li, 66, ambaye ni mhariri wa gazeti la China Youth Daily alisema kwa lugha ya Kiingereza.

Li alipata umaarufu kimataifa, alipokitaka chama cha National People’s Congresss (NPC), kupinga marekebisho hayo ya katiba.

Kupitia barua ya wazi aliyoiandika wiki jana, mhariri huyo alionya kuwa hatua hiyo “itapanda mbegu ya uhasama ya fujo nchini China.”

“Msipojitokeza wazi wazi na kupinga hatua hii, watadhani kwamba sote twakubaliana nao,” Li akaambia shirika la habari la AFP.

Barua hiyo iliibua msisimko mkubwa miongoni mwa Wachina kwenye mitandao ya kijamii wiki jana, hali iliyopelekea kuzima mjadala kuhusu suala hilo.

Dai kuwa umma unaunga mkono hatua hiyo, kwa kauli moja, liko kwenye taarifa ya marekebisho yaliyopendekeza katika kikao cha ufunguzi wa mkutano wa kila mwaka wa NPC mnamo Jumatatu. Wabunge wote wameelezea imani kwamba watapiga kura ya “ndio” mnamo Jumapili.

Lakini watu wengi nchini China- kuanzia wafanyabiashara, makundi ya akina mama, walimu, viongozi wa kidini na maafisa wastaafu- wamepinga hatua hiyo kupitia mitandao ya kijamii na mahojiano na wanahabari wa kigeni.

You can share this post!

SHANGAZI AKUJIBU: Nilifumania mke nikamuacha, wa zamani...

Serikali inabagua wabunge wanawake wa NASA – Passaris

adminleo