• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 6:55 AM
Mbunge akamatwa kwa kuongoza maandamano msituni Mau

Mbunge akamatwa kwa kuongoza maandamano msituni Mau

Na GEORGE SAYAGIE

MBUNGE wa Emurrua Dikirr, Johanna Ngeno amekamatwa ndani ya Maasai Mau baada ya kuongoza maandamano kupinga watu kufurushwa kutoka msitu wa Mau.

Mbunge huyo alikuwa anaongoza maandamano kupinga awamu ya pili ya ufurushaji watu kutoka kwa msitu huo eneo la Siarra Leone (Sierra Leone) Jumanne alipokamatwa na diwani wa wadi ya Segemian walipokuwa wakitembea na wakazi hao wanaoishi ndani ya msitu huo kinyume cha sheria.

Wawili hao wamepelekwa katika Kituo cha Polisi cha Narok kuandikisha taarifa.

 

 Tunaandaa habari kamili…

You can share this post!

Nyumba 60 zateketea Mukuru-Kayaba

FUNGA-KAZI: Muhula wa uhamisho wafungwa rasmi Ulaya

adminleo