• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Mabwanyenye wachache wanamiliki 80% ya utajiri Nairobi na Mombasa – Utafiti

Mabwanyenye wachache wanamiliki 80% ya utajiri Nairobi na Mombasa – Utafiti

Na BERNARDINE MUTANU

WAKAZI wachache wa Nairobi na Mombasa ndio matajiri zaidi nchini Kenya kulingana na utafiti wa hivi punde.

Utafiti huo, Kenya Integrated Household Budget Survey (KIHBS), ulipata kuwa asilimia 20 ya wakazi wa Nairobi na Mombasa wanamiliki asilimia 86.4 na 78.2 kwa mpangilio huo, ya utajiri wa maeneo hayo.

Hii ni kumaanisha zaidi ya asilimia 80 ya wananchi wanaoishi katika miji hiyo wana mapato ya chini zaidi.

Jijini Nairobi, asilimia 40 ya wakazi wa Nairobi ni maskini kupindukia kulingana na utafiti huo, na uwezo wao wa matumizi ya fedha ni asilimia 0.4 pekee.

Asilimia 60 ya wananchi wote nchini wana uwezo wa kutumia asilimia 2.7 ya mapato ya taifa, kumaanisha asilimia 40 ya wananchi wote wanatumia asilimia 97.3 ya rasilimali ya taifa.

Katika eneo la Mombasa, asilimia 60 ya wakazi wamedhibiti asilimia 4.7 ya rasilimali jijini humo.

Utafiti huo ulionyesha kuwa kuna tofauti kubwa zaidi ya kimapato kati ya wananchi huku wale tajiri zaidi wakipatikana katika maeneo ya miji ambako mapato hayalingani.

Huku wachache wakindeelea kwa utajiri, wengi zaidi wanazidi kuumizwa na umaskini.

Asilimia 60 ya rasilimali ya Kenya inamilikiwa na watu wachache zaidi (milioni 9) ilhali 36,296,000 wamesalia kuwa maskini kuambatana na makadirio ya idadi ya wananchi ya 2016.

Tofauti za kimapato zimejitokeza zaidi katika maeneo ya miji ikilinganishwa na maeneo ya mashambani.

You can share this post!

Twitter yajiunga na Google na Facebook kuharamisha...

Mahakama yaagiza Miguna aachiliwe mara moja

adminleo