• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Kuria apokelewa vizuri Nyanza baada ya muafaka

Kuria apokelewa vizuri Nyanza baada ya muafaka

NA PETER MBURU

MUAFAKA baina ya mkono kati ya Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga umewanusuru viongozi wengi waliochukiwa na wafuasi wa mirengo hasimu, huku baadhi yao wakiishia kuwa mabingwa katika maeneo ya wafuasi wa waliokuwa maadui mbeleni.

Baadhi ya viongozi walionufaika na salamu hiyo muhimu kwa taifa ni mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria, ambaye siku chache zilizopita ametembelea maeneo mengi yaliyo ngome za upinzani.

Bw Kuria ambaye mbeleni alikosolewa vikubwa na wadadisi na wafuasi wa Bw Odinga sasa anatembea sehemu za Nyanza na Magharibi kama nyumbani kwake, akila na kuimba na waliomwona kama hasimu mkubwa mbeleni.

Ziara hizo, aidha zimemsaidia kiongozi huyo kueneza ajenda ya haja ya sehemu hizo ambazo kwa miaka mingi zimetofautiana kisiasa na eneo la Mlima Kenya kushirikiana na eneo hilo na kujikomboa kutoka upinzani.

“Tumeanza safari ya ugatuzi wa salamu. Wakati wa siasa umeisha na tunaona nchi yote iko na amani, hata uchumi utaimarika na wawekezaji sasa wanaona umuhimu wa salamu hiyo,” mbunge huyo akaeleza alipokuwa akizungumzia watu Homabay.

Ziara hizo, hata hivyo, zimeonekana kama zinazonuia kukijengea chama cha Jubilee sifa na kukipa hatua, kabla ya uchaguzi wa 2022.

“Mambo ya upinzani hamuwezani nayo, kwani hata kipawa chake hamna, tuungane pamoja ili twende safari hii pamoja kwani nyumba ya Jubilee ni kubwa,” Bw Kuria akasema alipokuwa akihutubia watu Kakamega.

You can share this post!

Madoya ahakikishia Zoo kuwa itasalia ligini

Moi aombe familia ya Matiba msamaha kwa mateso –...

adminleo