• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Saidieni shule za kibinafsi zisifilisike, Magoha awarai wazazi

Saidieni shule za kibinafsi zisifilisike, Magoha awarai wazazi

WIZARA ya Elimu imewarai wazazi wenye uwezo kifedha kuwasaidia walimu wa shule za kibinafsi, ili shule hizo zisifilisike kutokana na janga la virusi vya corona.

Waziri wa Elimu, Prof George Magoha, alisema wazazi wajitolee kukubaliana na shule za kibinafsi ambako wanao wanasomea kuhusu jinsi wanaweza kuchangia gharama za mahitaji ya shule wakati huu zimefungwa.

Walimu wengi katika shule hizo hawajakuwa wakipokea mishahara tangu Machi wakati shule zilifungwa kutokana na virusi, huku shule nyingine zikihofiwa kufungwa kwa sababu kuna madeni yanayostahili kulipwa.

Akizungumza Jumamosi alipokagua Chuo cha Mafunzo ya Walimu cha Asumbi, Kaunti Ndogo ya Rangwe, Kaunti ya Homa Bay kuhusu kiwango cha kujiyayarisha kwake, waziri alisema shule hizo huwa zinawaajiri zaidi ya walimu 135,000 ambao wako katika hatari ya kupoteza ajira, ikiwa waajiri wao wataamua kuzifunga shule kutokana na ukosefu wa fedha.

“Wazazi wanapaswa kuungana kuhakikisha kuwa shule hizo hazisambaratiki kutokana na hali iliyopo,” akasema.

Na George Odiwuor

You can share this post!

Baraza jipya la wazee kubuniwa Mlima Kenya

Wanachuo wasusia masomo mtandaoni

adminleo