Kimataifa

Maafisa sita wa usalama washtakiwa kupanga kumng’oa Rais Tinubu wa Nigeria

Na REUTERS April 22nd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

ABUJA, Nigeria:

SERIKALI ya Nigeria Jumatano iliwasilisha mashtaka matatu ya uhalifu dhidi ya maafisa sita wa zamani wanaoshutumiwa kwa jaribio la kupindua serikali ya Rais Bola Tinubu mwaka jana.

Stakabadhi ambazo ziliwasilishwa kortini zitatumika kumshtaki jenerali wa kijeshi aliyestaafu pamoja na wenzake kwa kosa la uhaini na kufadhili ugaidi.

Mshukiwa wa saba ambaye ni gavana wa jimbo bado anaandamwa ili naye ashtakiwe kwa uhaini.

Mwanasheria Mkuu na Waziri wa Haki Lateef Fagbemi waliwasilisha kesi hiyo mnamo Jumatatu kwenye mahakama ya Abuja. Washukiwa hao walishtakiwa hapa jana.

Kesi hiyo ya uhaini inaonyesha jinsi Tinubu aliyechukua mamlaka mnamo 2023 analenga kuhakikisha usalama na udhabiti wa serikali yake.

Hii ni kwa sababu ukosefu wa usalama umekuwa ukishuhudiwa sana kaskazini mwa Nigeria na pia kuna uhasama wa kisiasa kati ya mirengo mbalimbali na uchumi wa taifa hilo pia unayumbayumba.

Mnamo Oktoba mwaka jana, Rais Tinubu alifanya mabadiliko kwenye jeshi na kuweka mwandani wake kukabili maasi na pia matukio ya utovu wa usalama.