• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 1:47 PM
Uwanja wa JKIA watambuliwa kwa ubora Afrika

Uwanja wa JKIA watambuliwa kwa ubora Afrika

Na BERNARDINE MUTANU

UWANJA wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) uliorodheshwa kama uliofanya vyema zaidi katika bara la Afrika.

Kulingana na utafiti uliofanywa na Baraza la Viwanja vya Ndege (ACI), shirikisho la viwanja vya ndege ulimwenguni, JKIA ndio uwanja ulioimarika zaidi katika eneo hili.

JKIA iliorodheshwa katika kwa kiwango hicho kutokana na huduma kwa wateja kutokana na maoni yao.

Kulingana na Mamlaka ya Kusimamia Viwanja vya Ndege (KAA) hiyo ilikuwa ishara njema wakati ambapo uwanja huo unazidi kufanyiwa marekebisho.

“Kutambuliwa kwetu kunaonyesha kuwa mikakati ambayo imewekwa kuimarisha huduma inazaa matunda. Ninaamini kuwa tuko kwa njia sambamba,” alisema mwenyekiti wa KAA, Jonny Anderson katika taarifa.

You can share this post!

EABL yalenga kuunda lita milioni 100 za ‘Keg’...

KCB yasema kiwango cha riba kimeipunguzia mapato

adminleo