• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:23 PM
Iran yateketeza bendera ya Amerika bungeni

Iran yateketeza bendera ya Amerika bungeni

AFP na CHARLES WASONGA

WABUNGE wa Iran walitekeza bendera ya Amerika huku wakiimba “Kifo kwa Amerika” Jumatano ndani ya bunge la taifa hilo.

Walikuwa wakipinga uamuzi wa Rais wa Amerika Donald Trump wa kuondoa taifa lake kutaka mkataba wa kinyuklia unaoshirikisha mataifa kadha.

Picha zilizopeperushwa katika vyombo kadha vya habari nchini Irani zilionyesha mbunge mmoja akipeperusha kijibendera kabla ya kukiteketeza ndani ya ukumbi wa bunge.

Mojtaba Zolnour ambaye ni mbunge wa chama cha Conservative naye mbunge huyo na kuteketeza nakala ya mkataba huo wa kinuklia.

Wabunge wengine waliungana nao wakiimba, “Kifo cha Amerika”, kauli ambayo imeshika kasi miongoni mwa wabunge wa Conservative.

“Mjihadhari msiteketeze bunge,” Spika Ali Larijani alisema.

Maafisa wakuu nchini Iran wamelaani uamuzi wa Trump kuiondoa Amerika katika mkataba huo uliotiwa saini mwaka wa 2015.

Kutiwa saini kwa mkataba huo kulipelekea kuondolewa kwa vikwazo dhidi ya Iran kwa makubaliano kwamba isitishe shughuli za utengenezaji zana za kinyuklia.

Wakati huo huo, mataifa ya bara Uropa yenye uwezo kiuchumi Jumatano yalijitahidi kuokoa mkataba huo baada ya Trump kuondoa Amerika kutoka kwayo na kurejesha vikwazo dhidi ya Iran.

Hatua hiyo ya Trump ilishutumiwa na mataifa kadha ya ulimwengu, kwani huenda ikapelekea ongezeko la fujo katika eneo la Mashariki ya Kati.

Trump aliukosoa mktaba huo wa 2015 kwenye hotuba aliyotoa Jumanne akiwa katika Ikulu ya White House.

You can share this post!

Mbinu ilizotumia Safaricom kuzoa faida ya Sh55 bilioni...

Pasta amfurusha mke kwa kutisha kusambaratisha kanisa

adminleo