• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 8:55 AM
Mashoga 6,000 hatarini kuambukizwa HIV kuliko makahaba

Mashoga 6,000 hatarini kuambukizwa HIV kuliko makahaba

Na CHARLES LWANGA

KARIBU watu 6,000 wanofanya ushoga mjini Malindi wako katika hatari ya kuambukizwa na virusi vya Ukimwi kutokana na ongezeko la vijana wanaofanya biashara ya ushoga katika mji huo wa kitalii.

Mtaalamu wa maswala ya Ugonjwa wa Ukimwi katika hospitali ya Malindi, Dkt Godfrey Njoroge, alisema idadi hiyo imeongezeka kutokana na ukosefu wa ajira.

“Kulingana na utafiti, karibu watu 6,000 wanakisiwa kufanya mapenzi na wanaume wenzao na nambari hiyo huenda ikawa kubwa ikilinganishwa na idadi ya wanawake wanaofanya ukahaba mjini humu,” alisema.

Akizungumza na wanahabari mjini Malindi, aliitaka serikali kupitia mashirika yasiyo ya kiserikali wagawe mipira za kondomu na mafuta kwa mashoga hao ili ipunguze usambazaji ukimwi mjini humo.

“Kama unavyofahamu, sehemu inayotumiwa haikuumbwa kwa ajili ya kufanyia mapenzi na kwa hivyo ni mahali ambapo virusi vya ukimwi vinaweza kuigilia kwa urahisi wakati wa mapenzi,” alisema.

Dkt Njoroge alisema wateja wao ni watu matajiri mjini Malindi na watalii wanaozuru mji huo kwa likizo.

Bi Evans Onyango, ambaye pia ni mtaalamu wa janga la Ukimwi hospitalini humo aliwasihi watu wanaofanya ushoga watembelee vituo vya afya ili wapime hali yao ya virusi vya HIV wapate madawa.

“Baadhi yao hawapendi kwenda hospitali kupimwa na ingekuwa vyema waje hospitali ili tuweze kuwasaidia,” aliongeza.

Kulingana na Shirika la kupambana na janga la Ukimwi nchini, uambukizaji wa Ukimwi katika Kaunti ya Kilifi iko katika asilimia 4.2, kumaanisha kuwa katika kila watu 100 wanne wao wanabeba virusi vya Ukimwi.

 

You can share this post!

Shule mbioni kupaka mabasi rangi ya manjano muda ukiyoyoma

Mwaka mmoja baada ya Wamakonde kutambuliwa, bado ni kilio

adminleo