• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 8:50 AM
Kipa Sergio Romero kati ya wachezaji wanane ambao wameondoka Man-United

Kipa Sergio Romero kati ya wachezaji wanane ambao wameondoka Man-United

Na MASHIRIKA

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

KIPA raia wa Argentina, Sergio Romero, ameagana rasmi na Manchester United ambao watashiriki mazungumzo na kiungo veterani Juan Mata, 33 kuhusu uwezekano wa mktaba wake kurefushwa ugani Old Trafford.

Romero, 34, hajawajibikia Man-United tangu Agosti 2020 baada ya kurejea kwa Dean Henderson aliyekuwa ametumwa Sheffield United kwa mkopo wa msimu mmoja.

Mata ambaye ni raia wa Uhispania ana hadi Juni 30, 2021 kukataa au kukubali ofa mpya atakayopokezwa na Man-United ambao wamejivunia huduma zake ugani Old Trafford kwa kipindi cha miaka saba iliyopita.

Jumla ya wanasoka wanane wameachiliwa rasmi na Man-United kuondoka ugani Old Trafford muhula huu.

Kipa chipukizi Joel Pereira, 24, amejiengua kambini mwa mabingwa hao mara 20 wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) huku usimamizi ukitarajiwa kujadili zaidi kuhusu mustakabali wa kipa mkongwe Lee Grant, 38.

Beki Max Taylor, 21, aliyepona saratani mnamo 2018 ameruhusiwa pia kuondoka ugani Old Trafford. Nyota huyo alichezeshwa mara ya mwisho mnamo 2019 katika gozi la Europa League dhidi ya Astana ya Kazakhstan.

Mata alisajiliwa na Man-United kutoka Chelsea kwa kima cha Sh5.1 bilioni. Hata hivyo, alichezeshwa mara tisa pekee kwenye kampeni za EPL mnamo 2020-21.

  • Tags

You can share this post!

Moraa atesa mbio za mita 800 nchini Finland kinadada...

Stoke City warefusha mkataba wa kiungo Obi Mikel kwa mwaka...