NA CHARLES WASONGA
MWAKILISHI wa Kenya katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) Kanini Kega jana Alhamisi alifurushwa kutoka kwa mkutano wa kisiasa na vijana wanaounga mkono Katibu Mkuu aliyeondolewa mamlakani Jeremiah Kioni.
Bw Kega, ambaye juzi alitangaza kufanya kazi na muungano wa Kenya Kwanza, chini ya Rais Ruto, aliondolewa kutoka mkutano huo jijini Nairobi.