NA RICHARD MUNGUTI
CHAMA cha Wanasheria Nchini (LSK) kimewasilisha kesi kupinga utekelezaji wa Sheria ya Fedha, 2023 inayoshurutisha waajiri kukata wafanyakazi asilimia 1.5 ya mishahara.
Waajiri pia wanatakiwa watoa kiwango sawa na hicho cha kila mfanyakazi.
LSK inaasema sheria hii inakandamiza haki za wafanyakazi na waajiri.