• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 6:46 PM
Beki chipukizi wa Arsenal William Saliba kujiunga na Nice ya Ufaransa kwa mkopo

Beki chipukizi wa Arsenal William Saliba kujiunga na Nice ya Ufaransa kwa mkopo

Na MASHIRIKA

BEKI chipukizi wa Arsenal, William Saliba anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake hadi Nice kwa mkopo hadi mwishoni mwa msimu huu.

Sogora huyo mwenye umri wa miaka 19 alijiunga na Arsenal mnamo 2019 kwa kima cha Sh3.8 bilioni kabla ya kudumishwa kambini mwa Saint-Etienne kwa mkopo wa mwaka mmoja.

Tangu wakati huo, amekuwa akiwajibishwa katika kikosi cha chipukizi wasiozidi umri wa miaka 21 kambini mwa Arsenal na hajawahi kupangwa katika kikosi cha kwanza cha watu wazima.

Kwa kutumwa Nice, ni matarajio ya Saliba kwamba atapata muda wa kutosha wa kuwajibishwa uwanjani kabla ya kurejea kuwa tegemeo la Arsenal waliomtwaa kwa mkataba wa miaka mitano kutoka St-Etienne.

Kufikia sasa Nice wanashikilia nafasi ya 12 kwenye msimamo wa jedwali la Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1).

  • Tags

You can share this post!

Mwanasoka wa zamani wa Man-United, Darren Fletcher, arejea...

Vinara wa KRU wakuna vichwa katika juhudi za kufanikisha...