• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
Familia ya Glazer kuuza hisa 9.5 milioni za Man-United kwa Sh21.4 bilioni

Familia ya Glazer kuuza hisa 9.5 milioni za Man-United kwa Sh21.4 bilioni

Na MASHIRIKA

WAMILIKI wa Manchester United wametoa fursa kwa mashabiki wao kujinunulia hisa 9.5 milioni za thamani ya Sh21.4 bilioni.

Mabingwa hao mara 20 wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) walitaarifu Soko la Hisa la New York kuhusu mauzo ya hisa hizo kwa majina ya wakurugenzi wa klabu Kevin Glazer na Edward mnamo Oktoba 5, 2021.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hakuna mafao yoyote ambayo Man-United itapata kutokana na mauzo ya hisa hizo.

Man-United ilitoa tangazo hilo miezi mitano baada ya mechi yao ya EPL dhidi ya Liverpool kuahirishwa kutokana na vurugu na fujo za waliokuwa wakilalamikia maamuzi ya vinara kuingiza kikosi kwenye kipute kipya cha European Super League (ESL). Joel Glazer ambaye ni mmoja kati ya wenyeviti wa Man-United alihusika pakubwa katika mchakato wa kujumuisha kikosi chake kwenye ESL.

Mnamo Machi 2021, Avram Glazer aliuza hisa nyingine za thamani ya Sh10.9 bilioni katika kikosi cha Man-United. Jumla ya hisa zote ambazo sasa zinauzwa na Man-United ni asilimia nane pekee ya zile zinazomilikiwa na familia ya Glazer ambayo kwa sasa imesalia na asilimia 69 ya hisa.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Vipusa wa Barcelona wapokeza Arsenal kichapo cha kwanza...

Sutton athubutu kusema Salah anapiku Ronaldo na Messi...