Na MASHIRIKA
WENYEJI Japan waliwakomoa Mexico 2-1 mnamo Jumapili jijini Tokyo na kusajili ushindi wao wa pili kwenye Olimpiki zinazoendelea.
Mabao ya Japan yalifungwa na Takefusa Kubo na Ritsu Doan.
Japan ambao kwa sasa wanaselelea kileleni mwa Kundi A kwa alama sita, walishuka ulingoni wakijivunia kucharaza Afrika Kusini 1-0 katika mechi ya awali.
Katika Kundi B, Mikel Oyarzabal wa Real Sociedad katika Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) alisaidia Uhispania kupepeta Australia 1-0 siku tatu baada ya kulazimishiwa sare tasa na Misri.
Ujerumani waliopokezwa kichapo cha 4-2 kutoka kwa mabingwa watetezi Brazil katika mechi ya kwanza, walijinyanyua na kuwakung’uta Saudi Arabia 3-2 katika Kundi D.
Katika Kundi C, fowadi Chris Wood wa Burnley aliwachochea New Zealand kucharaza Honduras 3-2 huku Korea Kusini wakiwaponda Romania 4-0.
MATOKEO YA OLIMPIKI (Jumapili):
Ufaransa 4-3 Afrika Kusini
Japan 2-1 Mexico
New Zealand 2-3 Honduras
Romania 0-4 Korea Kusini
Misri 0-1 Argentina
Australia 0-1 Uhispania
Brazil 0-0 Ivory Coast
Saudi Arabia 2-3 Ujerumani
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO