• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 6:50 AM
Sancho afanyiwa vipimo vya afya kabla ya kuingia katika sajili rasmi ya Manchester United

Sancho afanyiwa vipimo vya afya kabla ya kuingia katika sajili rasmi ya Manchester United

Na MASHIRIKA

FOWADI Jadon Sancho wa timu ya taifa ya Uingereza amefanyiwa vipimo vya afya kadri anavyojizatiti kukamilisha uhamisho wake kutoka Borussia Dortmund ya Ujerumani hadi Manchester United ya Uingereza kwa kima cha Sh11.4 bilioni.

Man-United na Dortmund waliafikiana kuhusu uhamisho wa Sancho, 21, mnamo Julai 1. Hata hivyo, maagano hayo yalikuwa yarasimishwe mwishoni mwa kampeni za Euro mwaka huu.

Sancho aliwasili katika uwanja wa Carrington ambao hutumiwa na Man-United kwa mazoezi mnamo Julai 13. Alifanyiwa vipimo vya afya kabla ya kamera kumnasa akiondoka kwa gari.

Man-United wanatarajiwa kumtambulisha rasmi Sancho kwa mashabiki wao wakati wowote wiki hii.

Sancho, Bukayo Saka na Marcus Rashford walirushiwa cheche za matusi na kubaguliwa mitandaoni kwa msingi wa rangi ya ngozi zao baada ya kupoteza mikwaju ya penalti wakati wa fainali ya Euro iliyokutanisha Uingereza na Italia mnamo Julai 11, 2021 katika uwanja wa Wembley jijini London.

Ingawa Sancho alikuwa mchezaji mwenza wa Phil Foden uwanjani Etihad kabla ya kuhamia Dortmund mnamo 2017, sogora huyo hakuwajibishwa katika mchuano wowote wa kikosi cha kwanza cha Man-City.

Mechi ya pekee ya haiba kubwa ambayo Sancho alishiriki nchini Uingereza ni kipute cha Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kilichoshuhudia Dortmund wakipepetwa na Tottenham Hotspur mnamo Februari 2019 uwanjani Wembley.

Sancho alikosa michuano yote ya mikondo miwili iliyosakatwa na Dortmund kwenye robo-fainali za UEFA mnamo 2020-21.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

LSK yataka afisa apewe dhamana kabla ya kunaswa

BURUDANI: Matamanio ya Dizo Cappy ni kunguruma ndani ya WCB...