• Nairobi
  • Last Updated March 18th, 2024 8:55 PM
Uhuru atandika Ruto 3-0

Uhuru atandika Ruto 3-0

Na BENSON MATHEKA

MPANGO wa Naibu Rais William Ruto (kwenye picha) kushindana na Rais Uhuru Kenyatta kudhibiti jiji kuu la Nairobi umetibuka baada yake kuzidiwa maarifa.

Hii ni baada ya Rais Kenyatta hapo jana kusambaratisha uchaguzi mdogo uliopangwa kufanyika Februari 18, kufuatia kutimuliwa kwa Gavana Mike Sonko.

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ilipotangaza tarehe ya uchaguzi mdogo, Rais Kenyatta alitafuta mbinu za kuuepusha kwa kuchukua fursa ya uteuzi wa naibu gavana, Bi Ann Kananu Mwenda, aliofanya Bw Sonko mwaka jana lakini ukakosa kuidhinishwa kutokana na agizo la mahakama.

Mikakati ya Rais Kenyatta ilikuwa ni kuhakikisha Bi Kananu ameidhinishwa na bunge la kaunti kwa wadhifa huo na kuapishwa. Hapo jana, mipango ya mrengo wa Rais Kenyatta ilifikia kilele kwa bunge la kaunti kuidhinisha uteuzi wa Bi Kananu, ambaye muda mfupi baadaye aliapishwa kuwa Naibu Gavana.

Kuapishwa kwake kunamaanisha kuwa mipango ya Dkt Ruto, aliyeunga mkono aliyekuwa mbunge wa Starehe Askofu Margaret Wanjiru imesambaratika.

Hii ni kwa sababu akiwa Naibu Gavana, Bi Mwenda ataapishwa kuwa gavana wakati wowote kuanzia sasa.Nairobi imekuwa bila naibu wa gavana tangu 2018 wakati Polycarp Igathe alipojiuzulu akilalamikia kuhangaishwa na Bw Sonko, na uteuzi wa Bi Kananu kupingwa mahakamani mwaka jana.

Hatua hiyo ilifanya kukosekana mtu wa kujaza nafasi ya Bw Sonko.Uchaguzi huo ungegharimu mabilioni ya pesa na kuzua changamoto za kuzuia kuenea kwa Covid-19, pamoja na kutishia kinyang’anyiro ambacho kingeaibisha Rais Kenyatta iwapo mgombeaji wa Dkt Ruto angeshinda.

Tukio hilo la jana ni pigo kubwa kwa Dkt Ruto ambaye amekuwa akipasha misuli moto akijiandaa kumenyana na Dkt Ruto alikuwa akimuunga mkono Bi Wanjiru kuwania kiti hicho kwa tiketi ya chama kipya cha United Democratic Alliance (UDA).

Upande wa Rais Kenyatta ulianza mikakati ya kuepusha uchaguzi mara baada ya Bw Sonko kung’atuliwa mwezi uliopita, kwa kuhakikisha kwanza kesi iliyowasilishwa na Peter Agoro akipinga Bi Kananu kupigwa msasa na bunge imeondolewa mahakamani.

Chama cha Thirdway Alliance baadaye kiliwasilisha kesi kupinga shughuli hiyo lakini ikatupiliwa mbali hapo jana asubuhi, na hivyo kupisha Bi Kananu kuhojiwa na kuapishwa.

Mnamo Alhamisi, Mahakama Kuu nayo ilisimamisha uchaguzi wa ugavana Nairobi hadi kesi za kupinga kuondolewa ofisini kwa Bw Sonko zisikilizwe na kuamuliwa, jambo ambalo lina uwezekano mkubwa wa kupitwa na wakati.

SHUGHULI KUHARAKISHWA

Katika moja ya shughuli zilizochukua muda mfupi zaidi katika historia ya mabunge ya kaunti tangu ugatuzi uanze nchini mnamo 2013, kamati ya uteuzi iliyo na washirika wa Rais Kenyatta ilimhoji Bi Mwenda asubuhi, ikawasilisha jina lake katika kikao cha madiwani wote, kikapitisha bila kupingwa na kisha akaapishwa naibu gavana dakika chache baadaye nje ya jumba la mikutano la KICC.

mwaniaji ambaye angeteuliwa na mrengo wa Rais Kenyatta.Sasa Dkt Ruto ameachwa kupambana na vinara wa NASA katika chaguzi ndogo za Machakos (useneta) na ubunge katika Matungu na Kabuchai.

Baada ya kushinda ODM katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa Msambweni iliyo Kaunti ya Kwale na udiwani wa Gaturi katika Kaunti ya Murang’a mwaka jana, Dkt Ruto na mrengo wake wa Tangatanga wamekuwa na ujasiri wa kupimana na vigogo wengine wa siasa katika ngome zao.

You can share this post!

Bobi Wine asema majeshi yameteka nyumba yake, serikali...

Museveni angali mbele Bobi Wine akisisitiza wanajeshi...