• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 5:10 PM
Aunda programu za kompyuta kuifaa mikahawa

Aunda programu za kompyuta kuifaa mikahawa

Na MAGDALENE WANJA

Bw Dennis Omito alizaliwa na kulelewa mjini Nanyuki karibu na kambi za kijeshi ambapo aliweza kuona ndege za wanajeshi mara kwa mara.

Hii ilimfanta kuwa na hamu sana ya kutaka kuwa rubani, na punde tu alipomaliza masomo yake, aliweza kusomea urubani. Alipata ujuzi wa kue desha ndege aina ya Cessna C15.

Hata hivyo, Omito anasema kuwa alijifunza hayo yote ili kujifurahisha na kutimiza kama moja wapo ya malengo yake maishani.

Kando na hayo, alipenda sana ufundi wa kutengeneza programu za kompyuta na simu.

Alipofuzu na cheti cha stashahada katika mafunzo Sayansi ya Kompyuta mnamo mwaka 2004, alipata kazi katika kampuni ya CMC Motors Group Ltd ambako alifanya kazi kwa muda wa miaka miwili katika cheo cha Computer Programmer.

“Baada kufanya kazi hio kwa muda wa miaka miwili, nikiweza kupata nafasi nyingine katika kampuni ya Toyota East Africa Ltd.

Alipokuwa pale, aliweza kujifunza mengi kuhusu biashara, na baada ya miaka mitatu, alijiuzulu na kuendeleza masomo ya kirubani.

Masomo hayo yalimchukua muda wa mwaka mmoja kisha ajarejelea kazi yake ya kuunda programu.

Alifanya kazi hio kama mshauri wa kampuni kubwa nchini kama vile Verve KO Ltd, amebaki aliweza kutengeneza program ya1963 Matatu Cashless platform, ambayo ilizinduliwa na Rais Uhuru Kenyatta.

“Mnamo mwaka 2016, nilizindua kampuni yangu kwa Jina e-ofisi Technology Limited ambayo niliendesha kwa ushirikiano na mke wangu Martha Omito,” aliongeza.

Kupitia kampuni hio, ameweza kuunda programu kadhaa ikiwemo ile ya hivi punde ya BizWiz POS na ERP System.

Hii ni programu ambayo inatumika na baadhi ya hotel na mikahawa mkubwa ili kuleta pamoja shughuli zote za kibiashara pamoja.

Omito mwenye umri wa miaka 37 anasema kuwa programu hii ni tofauti na zile za hapo awali amabazo baadhi ya hoteli na mikahawa huzitumia ambazo ni miigo ya zile za ulayani.

“Niliunda program hii mnamo mwezi Juni 2017 baada ya kupatana na mteja ambaye alitaka programu ambayo ni tofauti na zile za ulaya,” aliongeza Omito.

Aliongeza kuwa program hii huwezesha mmiliki wa biashara kueza kufuatilia rekodi zote kupitia kurasa hio kwa urahisi.

Baadhi ya mikahawa na hoteli ambazo zinatumia program hii ni pamoja na The Tunnel iliyoko eneo la Mombasa Road, The Curve By the Park iliyoko karibu na mbuga ya wanyama ya Nairobi, Ziwa Beach Resort iliyo eneo la Bamburi Mombasa, Dari Restaurant – Ngong Road na Brew Bistro Tap Room- Ngong Road.

Kupitia muundo huo, ameweza pia kuunda program nyingine ambayo inatumika kanisani.

“Wafuasi wanaweza kufuatilia matukio kanisani kama vile maombi,mahubiri na ata kutoa sadaka kupitia program hii,” alisema Omito.

Programu hii imekuwa na manufaa zaidi wakati wa mkurupuko wa maradhi ya Covid-19 mwaka mmoja uliopita.

 

You can share this post!

Ibrahimovic arejea kikosini akiwa na miaka 39

NCPB yaahidi kuboresha huduma kwa wakulima wa mahindi