• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
MAMA ashambuliwa na wanawe Homa Bay

MAMA ashambuliwa na wanawe Homa Bay

Na GEORGE ODIWUOR

Tafsiri: CHARLES WASONGA

MAMA mmoja na watoto wake wawili wamelazwa katika hospitali moja ya kibinafsi mjini Homa Bay baada ya kushambuliwa kwa upanga na mwanamume asiyejulikana nyumbani kwa Jumatatu usiku.

Mwanamke huyo aliyatambuliwa kama Mary Okiaka,51 alishambuliwa alipokuwa wakijaribu kumwokoa bintiye mwenye umri wa miaka 13 asijeruhiwa na mvamizi huyo.Ilidaiwa kuwa mvamizi huyo aliwakata kwa upanga mama huyo na wanawe wawili akilenga kuwaua.

Baada ya mpango wake kufeli, aligeukia ng’ombe wa familia hiyo na kumuua kwa kumkata kwa upanga.Maafisa wa usalama na wale wa utawala wangali wanajaribu kubaini sababu zilizochangia mwanamume huyo kushambulia familia hiyo.

Chifu wa kata ya Kabuoch Kapis Olala alisema wanakijiji walipiga ripoti katika afisi yake kwamba mshukiwa aliwavamia Mary na wanawe wakiwa usingizini.Mama huyo alishambuliwa kwa upanga kichwani alipokuwa akijaribu kumwokoa bintiye na mvamizi huo, kulingana na Chifu Olala.

“Mwanamke huyo na bintiye walipiga mayowe waliposhambuliwa. Mwanawe wa kiume naye alikuwa wakilala katika chumba kingine pia alifika kutaka kuokoa mamake na dadake. Lakini yeye pia akashambuliwa,” akasema afisa huyo wa utawala.

Bw Olala alisema mama huyo na wanawe wawili walipata majeraha kadha kichwani na sehemu zingine za mwili.Mshukiwa alitoroka baada ya kutekeleza unyama huo. Chifu Olala alisema anashirikiana na maafisa wa polisi kutoka Kituo cha Polisi cha Ndhiwa kuendesha uchunguzi kwa lengo la kumkamata mshukiwa.

  • Tags

You can share this post!

Kilio cha wazee wa MauMau Kirinyaga

SUPALIGI YA TAIFA: Coast Stima yapoteza mechi ya tatu...