NA WYCLIFFE NYABERI
WAZIRI wa Usalama wa Ndani Dkt Fred Matiang’i na katibu wa wizara hiyo Dkt Karanja Kibicho wamesema kelele za wakosoaji wao kuhusu kazi wanayoifanya haziwakoseshi usingizi.
Wakiongea Nyamira jana Ijumaa, walisema wamekuwa wakikosolewa na wanasiasa kwa kutekeleza majukumu yao ya kiserikali.