• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 2:29 PM
Mean Machine na Egerton Wasps waanza kufukuzia tiketi ya kuingia Kenya Cup

Mean Machine na Egerton Wasps waanza kufukuzia tiketi ya kuingia Kenya Cup

Na GEOFFREY ANENE

VITA vya kuamua timu zitakazoingia Ligi Kuu ya raga nchini (Kenya Cup) msimu 2021 vitang’oa nanga hapo Jumamosi wakati mabingwa wa zamani Mean Machine wataalika Egerton Wasps jijini Nairobi.

Machine ya Chuo Kikuu cha Nairobi, ambayo ilishinda Kenya Cup mwaka 1977, 1989 na 1990, ilitemwa misimu minne iliyopita baada ya kuvuta mkia kwenye ligi hiyo ya klabu 12. Mshindi kati ya Machine na Wasps ya Chuo Kikuu cha Egerton atajikatia tiketi ya kumenyana na Chuo Kikuu cha Masinde Muliro (MMUST) kutoka Kakamega katika nusu-fainali mnamo Februari 13.

Mchuano mwingine wa kufuzu kushiriki nusu-fainali kati ya timu ya Chuo Kikuu cha USIU na Northern Suburbs hautasakatwa baada ya USIU Martials kujiondoa mashindanoni. Inamaanisha kuwa Suburbs imeingia katika nusu-fainali jila jasho na itakabiliana na Leos ya Chuo Kikuu cha Strathmore.

Leos na MMUST zilikamilisha msimu wa kawaida wa 2019-2020 katika nafasi mbili za kwanza ambazo washikilizi wake huingia nusu-fainali moja kwa moja.

Mechi za kuwania tiketi ya kuingia Kenya Cup zitafuata masharti ya kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona. Mashabiki pia hawatakubaliwa uwanjani.

  • Tags

You can share this post!

Mamia ya wakazi Mukuru kupoteza makao kupisha ujenzi wa...

Klabu 19 kupigania taji la Ligi ya Taifa Daraja la Pili...