NA LAWRENCE ONGARO
AMPUNI ya Huduma za kidijitali ya Microsoft imetangaza ushirikiano na shirika la OCP Africa kwa minajili ya kuwainua wakulima wa chini wa Agro stakeholders katika bara la Afrika ifikapo mwaka wa 2025.
OCP Africa ambayo ni kitengo cha kampuni barani Africa husambaza mbolea kwa wakulima wa chini na itaendelea kushirikiana na kampuni ya Microsoft ili kukwamua wakulima na kuwapa mwongozo wa kisasa wa kilimo.
“Hii ni njia moja ya kuinua wakulima kupitia kilimo cha kidijitali katika bara la Afrika ili kukuza mazao yao,” alifafanua Bw Wael Elkabbany ambaye ni meneja mkuu wa masuala y kidijitali wa Microsoft katika bara la Afrika.nAlisema mpango huo italeta mabadiliko makubwa kwa wakulima na wataweza kujitegemea pakubwa katika upanzi wa chakula.
Aiyasema hayo katika mji wa Doha, nchini Qatar katika kongamano la tano la nchi inayoendelea huko.
Alisema mkutano huo kwa uumla ni muhimu kwa sababu itawapa wakulima ujuzi kamili wa kujitegemea kwenye kilimo hasa kupitia mbinu ya kidijitali.
Alisema wakulima wengi wakipata ujuzi huo wataweza kujitegemea na wataweza kujifanyia mambo yao bila kutegemea yeyote.