• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 4:55 PM
Mikopo: Wakenya wamchangia mwanaharakati

Mikopo: Wakenya wamchangia mwanaharakati

Na HILLARY KIMUYU

WAKENYA Ijumaa walimchangia mwanaharakati Mutemi wa Kiama dhamana ya Sh500,000.

Mwanaharakati huyo alikuwa ameachiliwa kwa dhamana na mahakama ya Nairobi baada ya hakimu kukataa ombi la upande wa mashtaka la kumzuilia kwa muda wa siku 14 ili kukamilisha uchunguzi.

Alishtakiwa kwa makosa ya kukaidi sheria za mtandao kuhusiana na kampeni ya Wakenya kwa IMF wakiitaka isikopeshe Kenya tena.

Kundi linalojiita Muungano wa Watetezi mtandaoni ndilo lilitoa wito kwa Wakenya waungane kumchangia Bw Kiama dhamana hiyo.

“Nawashukuru sana Wakenya. Muungano wa watetezi umehakikisha kuwa mwanaharakati huyo anaachiliwa huru. Lazima kama Wakenya tusimame imara na kuhakikisha tunapata haki na kulinda uhuru wa kujieleza,” akasema Bw Kiama.

Mwanaharakati huyo alishtakiwa kwa kuwa na mabango mawili yaliyoonya IMF dhidi ya kutoa mkopo kwa Wakenya hasa kwa Rais Uhuru Kenyatta na Naibu Rais Dkt William Ruto.

Korti pia ilimuonya Bw Mutemi dhidi ya kutumia akaunti zake za mitandaoni na awe akipiga ripoti kwa afisa wa uchunguzi kila siku hadi wakati kesi hiyo itakapotajwa Aprili 20, 2021.

“Hii notisi inaonya ulimwengu kwamba mtu ambaye picha yake na majina yake yapo kwenye bango hili haruhusiwi kushiriki biashara zozote kwa niaba ya raia wa Jamhuri ya Kenya.

“Taifa na vizazi vijavyo havitawajibikia kutokana na athari mbaya ya mikopo aliyochukua yeye,” ikasema notisi hiyo iliyomtia Bw Kiama matatani.

You can share this post!

UMBEA: Hakuna mpenzi mzuri au mbaya inategemea tu ikiwa...

Mipango kuandaa Muturi kuwania urais 2022 yaiva