• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 2:31 PM
Mwigizaji Lupita Nyong’o atangaza kutengana na mpenziwe raia wa Afrika Kusini

Mwigizaji Lupita Nyong’o atangaza kutengana na mpenziwe raia wa Afrika Kusini

NA LABAAN SHABAAN

MWIGIZAJI Lupita Nyong’o amefungua roho na kutangaza kutengana na mpenzi wake Selema Masekela.

Staa huyo alipasua mbarika ya utengano huo kupitia taarifa aliyochapisha kwenye ukurusa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram.

Nyota huyo wa filamu maarufu ya Black Panther aliweka paruwanja chanzo cha kitumbua chao kuingia mchanga kuwa ukosefu wa uaminifu.

“Kuna mambo mengi muhimu yanafanyika duniani sasa hivi, ninaomboleza na wanaoteseka. Wakati huu, ni muhimu kwangu kushiriki nanyi ukweli wa kibinafsi na mbele ya umma kujitenga na mtu nisiyemwamini tena,” Lupita alisema.

Kwenye chapisho refu mitandaoni, nyota huyo wa sanaa alikiri amekuwa katika msimu wa kuvunjwa moyo na anaamini yaliyomsibu yatakuwa somo kwa wengine wanaopitia matukio sawia.

“Ninajikuta katika msimu wa kuvunjwa moyo kwa sababu ya moto wa penzi unaozimwa vibaya na udanganyifu. Nimefikiria kukimbilia kwenye kivuli na kujificha lakini nimerudi kwenye mwanga na nimejipa nguvu ili niseme, kwa vyovyote vile, maisha yangu ni bora hivi,” alieleza.

Uchungu aliouhisi Lupita ulimfanya kufuta picha zote za Selema, ambaye ni mwana wa aliyekuwa mwimbaji tajika Afrika Kusini Hugh Masekela katika ukurasa wake wa Instagram huku aking’ang’ana kumfuta kwenye fikira zake.

Nyong’o na mtangazaji huyo wa runinga Masekela walitangaza uhusiano wao mara ya kwanza Disemba 2022 baada ya kuchumbiana gizani.

  • Tags

You can share this post!

Ruto: Yale mambo matatu kwa mafisadi na wafujaji wa mali ya...

Maswali mgeni wa heshima akikosa kufika Kericho kwa sherehe...

T L