• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 1:24 PM
Namuomba Mungu wa mwisho awe ni wewe – Hamisa Mobetto

Namuomba Mungu wa mwisho awe ni wewe – Hamisa Mobetto

Na MWANDISHI WETU

MWANAMITINDO wa Tanzania, Hamisa Mobetto ameandika ombi lake kuhusu mahusiano yake na mpenziwe.

Kwenye ujumbe wake, Mobetto alisema kuwa anamuomba Mungu mpenziwe Kevin Sowax awe wa mwisho huku akiambatanisha picha yao.

Mobetto ambaye amekuwa kwenye mahusiano na watu tajika ikiwemo, mwanamuziki Diamond Platnumz na Rick Ross, hajabahatika kudumu kwenye mapenzi nao.

Hata hivyo, tangu apatane na Sowax, mwanabiashara huyo ameonyesha kuridhika kwake na mapenzi huku akiomba heri na fanaka.

“Namuomba Mungu wa Mwisho Awe ni wewe @kevinsowax ????? ?,” akaandika.

Hata ingawa Mobetto na mwanamuziki wa rapu wa Amerika Rick Ross walikiri kutokuwa kwenye mahusiano, Ross aliwacha kumfuata Mobetto pindi tu alitangaza kuwa kwenye mahusiano.

Kabla kuonyesha uso wake mpenziwe, Mobetto aliposti gari aina ya Range Rover ambayo alikiri kuwa alinunuliwa na Sowax.

“Kuna wanaume, na kuna mwanamume wangu sasa. Asante sana mpenzi…niko karibu kulia. Asante kwa kunionyesha maana ya mapenzi ya kweli. Umekuwa jambo nzuri sana lililofanyika maishani,” akaandika.

Mobetto na Sowax walipatana nchini Uchina katika hafla ya kibinafsi na wamekuwa kwenye mahusiano kwa takribani miezi minne.

Kwenye mahojiano na wanahabari, Sowax alisema kuwa hakujuwa mpenziwe ni mtu maarufu walipopatana ila tu alivutiwa na uanabiashara wake na urembo.

  • Tags

You can share this post!

Uganda Airlines yalenga kuongeza safari zake Mombasa

Mumias: Bwanyenye Jaswant Rai aamua kuondoa kesi

T L