• Nairobi
  • Last Updated May 16th, 2024 8:50 PM
Ndege ya jeshi kusafirisha mwili wake Magoha

Ndege ya jeshi kusafirisha mwili wake Magoha

NA COLLINS OMULO

MWILI wa aliyekuwa Waziri wa Elimu, Prof George Magoha utasafirishwa kwa helikopta ya jeshi hadi kwao Yala, Siaya kwa mazishi wikendi ijayo.

Waziri wa ICT, Bw Eliud Owalo, alisema usafirishaji huo wa Alhamisi ni sehemu ya ahadi za serikali kwa familia ya marehemu.

“Tulitoa ahadi na tunaendelea kuzitimiza. Tutausafirisha mwili huo Ijumaa na kutoa usaidizi wowote utakaohitajika. Chakula tulichoahidi kimeshafika nyumbani,” akasema jana Jumatatu alipoongoza ujumbe wa serikali kutembelea waombolezaji jijini Nairobi.

Akiandamana na Katibu wa Usalama wa Ndani, Dkt Raymod Omollo na mbunge wa Gem Eisha Odhiambo, alisema ahadi zote zilizotolewa na Naibu Rais Rigathi Gachagua zimetimizwa.

Kwa mujibu wa ratiba, mwili wa Prof Magoha utazungushwa Nairobi kesho Jumatano ili kutazamwa na umma.

Alhamisi kutakuwa na misa ya wafu katika Consolata Shrine, Westlands, na Ijumaa usafirishwe kwa ndege hadi uwanja wa shule ya Msingi ya Yala.

  • Tags

You can share this post!

Bayern watandika Wolfsburg na kurejea kileleni mwa jedwali...

Polisi wasaka waliomuua kwa kisu mwanafunzi

T L