Na WINNIE ATIENO
SERIKALI inaharakisha kukamilishwa kwa miradi ya uwekezaji iliyoanzishwa na Rais Uhuru Kenyatta yenye thamani ya Sh1.4 trilioni katika eneo la pwani.
Miradi hiyo inalenga kuimarisha biashara, utalii na kuunda nafasi za ajira.
“Bandari ya Mombasa ni kituo muhimu cha kiuchumi humu nchini hivyo basi utendakazi wake una umuhimu mkubwa,” alisema Dkt Karanja Kibicho ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Kiufundi kuhusu Utekelezaji wa Maendeleo Nchini (NDITC).