• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 6:50 AM
TANZIA: Msanii wa TikTok afariki katika ajali ya barabarani Kericho

TANZIA: Msanii wa TikTok afariki katika ajali ya barabarani Kericho

NA VITALIS KIMUTAI

MWIGIZAJI mashuhuri katika mtandao wa kijamii wa Tiktok Kevin Oselu, almaarufu Baba Mona, na watu wawili walioaminika kuwa dada zake, wamekufa katika ajali mbaya iliyotokea katika barabara ya Londiani kuenda Muhoroni..

Ajali hiyo ilitokea Ijumaa jioni katika kituo cha kibiashara cha Tunnel, kata ndogo ya Marenfa, Kata ya Siwot, eneo bunge la Kipkelion Mashariki.

Walioshuhudia ajali hiyo walisema gari ndogo la kibinafsi lilipoteza mwelekeo na kugonga nguzo kando mwa barabara na kubondeka.

“Mtoto alirushwa nje ya gari hili ihala watu watatu wakapata majeraha kadhaa,” Bw Kiprotich Koech aliyeshuhudia ameambia Taifa Leo.

Ripoti zinasema kuwa mtoto huyo, anayeaminika kuwa bintiye Baba Mona, alikufa alipokuwa akikimbizwa katika hospitali ya karibu ya Fort Tennan.

Afisa wa polisi aliyefika katika eneo la tukio alisema watu wengine watatu walikufa papo hapo kutokana na majeraha.

“Inasemekana wanne hao ni watu wa familia moja ambao walikuwa wakisafiri hadi eneo la Kandege, Koru, kaunti ndogo ya Muhoroni katika mpaka wa kaunti za Kericho na Kisumu. Ninaweza kuthibitisha kuwa namjua mwanatiktok huyo na bintiye. Lakini siwajui abiria wengine,” afisa huyo wa polisi akasema.

“Baba Mona” alipata umaarufu kutoka kwa ushauri ambao aliwapa watu kupitia video kadha fupi alizoweka katika akaunti yake ya mtandao wa TikTok. Akaunti yake ilifuatiliwa na watu wengi.

Inasema kuwa alikuwa akisafiri kutoka Nairobi kuenda Kisumu ajali hiyo mbaya ilipotokea.

Polisi walipeleka maiti hizo katika hifadhi ya maiti ya hospitali ya St Vincent, iliyoko Kaunti ya Kericho.

Tafsiri: CHARLES WASONGA

  • Tags

You can share this post!

WANDERI KAMAU: Serikali ya Ruto ikome kutumia idara za...

NYOTA WA WIKI: Khvicha Kvaratskhelia

T L