• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
UGANDA: Demokrasia Afrika bado ni ndoto

UGANDA: Demokrasia Afrika bado ni ndoto

NA WACHIRA ELISHAPAN 

Bara la Afrika kwa Mara nyingine limejipata katika hali tata,baada ya rais wa jamhuri ya Uganda Yoweri Museveni kujipata kama mshindi wa uchaguzi wa urais  ulioandaliwa nchini humo.

Museveni alitabiriwa kuwa mshindi hapo awali hata kabla ya shughuli nzima za kuhesabu kura kukamilika. Ushindi wa Museveni hata hivyo ni kero kwa demokrasia ambayo inadhamini haki ya kila mwananchi hata akiwa mchanga,bila kumbagua kwa misingi ya rangi,Vcheo au hata tabaka.

Mgombeaji urais ambaye alionekana kuwa karibu sana na utepe wa kushinda almaarufu Bobi Wine kwa kweli hajakuwa akiishi kwa amani tangu atangaze azma yake ya kuwania urais, na badala yake amekuwa akijifuta machozi ya kukabiliana na polisi ambao waliaminika kutumwa na rais Museveni.

Mapema kabla ya kura kumalizika kuhesabiwa,Mwanaharakati huyo maarufu Bobi Wine alisikika akilalamika maafisa wa jeshi la Uganda walimzingira nyumbani kwake,wakidai kwamba walikuwa wanamlinda yeye.

Katika karne ya ishirini na moja,kuna uwezekano mkubwa Wananchi wanajua haki zao za kimsingi na hapo hawana uwezo mkubwa kuzitwaa,basi wanafanya kinyume na matarajio ya viongozi hao wanaowanyima haki zao.

Afrika huru inahitajika iwapo viongozi wanataka maendeleo na mataifa yaliyostawi. Hayati Rais mstaafu Daniel Moi alifanya kitendo ambacho daima kitakumbukwa na vizazi vingi cha kukubali kustaafu Mara tu alipoongoza taifa hili kwa miaka ishirini na minne,jambo ambalo liliashiria kwamba demokrasia ilikuwa imekwisha kukomaa nchini.

Inasikitisha zaidi kuwaona viongozi wenye Sera za kikoloni bado wakishikilia hatamu za uongozi katika karne hii. Tangu Kenya ilipojipatia katiba mpya mwaka wa 2010,iliashiria mwisho wa uongozi usio wa demokrasia,na hapo ikaashiria mwanzo wa uongozi wa mwananchi.

Tayari matunda ya ugatuzi kama vile usawa wa kijinsia,uongozi wa mihula miwili pamoja na ugavi sawa wa rasilimali za umma kwa hakika yameanza kutundwa.

Hivi majuzi Rais Kenyatta alikiri kwamba uongozi wa Kenya umekuwa ukishikiliwa na jamii mbili,akipendekeza kusema kwamba ni wakati wa jamii nyingine kuongoza taifa hili.

Semi za rais Kenyatta zinaashiria kwamba demokrasia imefika kiwango cha kushabikiwa na kukwezwa hadhi na mataifa yote bila kubagua. Bali na kubadili mfumo wa uongozi,kuna haja kubadili fikra kutoka kwa ukale usio na faida,hadi kwa usasa utakaofaidi watu wote.

Hivyo,umefika wakati mataifa yote ya kiafrika kuamka na kukana viongozi wanaojigandamiza kwenye nyadhifa za uongozi na kuwapa mamlaka wengine wenye maono tofauti.

You can share this post!

Watu 223 zaidi wapatikana na corona

Wakulima watakiwa kuwa wabunifu