NA CHARLES WASONGA
SIKU moja baada ya Rais Uhuru Kenyatta kutangaza kuwa serikali imetoa ruzuku kuchochea bei ya unga kupungua hadi Sh100 kutoka Sh210, wananchi Alhamisi walifurika katika maduka makubwa jijini Nairobi kununua bidhaa hiyo.
Uchunguza wa Taifa Leo ulibaini kuwa ni matawi ya dukakuu la Naivas pekee ndiyo yalikuwa yakiuza unga wa mahindi chapa Pembe kwa Sh99 kwa paketi moja ya kilo mbili.