NA PHILIP MUYANGA
MAHAKAMA Kuu imezuia kwa muda serikali ya Kaunti ya Kilifi kutoa pesa zilizoko kwenye akaunti za ushuru na zile za kuegesha magari.
Jaji Ann Ong’injo alitoa maagizo hayo baada ya kampuni ya Rain Drops Ltd, ambayo imekuwa ikichukua ushuru na kutoza ada za kuegesha magari kuwasilisha ombi.
Rain Drops Ltd inasema akaunti hizo zinafaa kubakia hivyo hadi kesi iamuliwe.