• Nairobi
  • Last Updated May 16th, 2024 8:50 PM
Askofu Anyolo amshukuru Papa kumkweza

Askofu Anyolo amshukuru Papa kumkweza

Na BRIAN OJAMAA

ASKOFU wa Jimbo la Kisumu, Philip Anyolo amemshukuru kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis kwa kumteua kama Askofu wa Nairobi akiahidi kuongoza vyema waumini wake.

“Jinsi mnavyojua mipango inaendelea ya kunihamisha kutoka Kisumu hadi Nairobi. Nimefurahia uteuzi huu na ninaahidi kuwa nitawatumikia waumini na mwenyezi Mungu kwa kujitolea sana,” akasema baada ya kuhudhuria mazishi katika eneobunge la Tongaren, Bungoma Kaskazini.

Alitoa wito kwa maaskofu wengine nao pia waendelee kumakinikia kazi ya Mungu akisema malipo yao mema yanawasubiri mbinguni.

Aidha, askofu huyo amekuwa akisimamia Shule ya Upili ya Bishop Anyolo katika eneobunge hilo kupitia miradi mbalimbali na sasa kuna matarajio mengi miongoni mwa wanafunzi na walimu baada ya kupandishwa kwake cheo.

Nao wakazi wa Tongaren walisifu uteuzi huo mpya wa Askofu Anyolo wakisema utasaidia kuvutia kanisa hilo waumini zaidi kutoka eneo hilo.

You can share this post!

UDAKU: CR7 amfunga Georgina hat-trick safi ya mapenzi

Mwanakijiji ajitolea kujenga barabara ya umma

T L