• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:55 AM
FUNGUKA: ‘Yote kwa raha zangu’

FUNGUKA: ‘Yote kwa raha zangu’

Na PAULINE ONGAJI

KATIKA ulimwengu wa uhuru wa kuchagua na kufurahia chochote kinachochochea mahaba, bila shaka hakuna nafasi ya kustaajabu.

Lakini hata ikiwa siku hizi ni vigumu kushangazwa na yanayojiri, bila shaka ukikumbana na ya Abe, 49, hutakuwa na budi ila kuachwa kinywa wazi.

Abe ni mhasibu mkuu katika shirika moja lisilo la kiserikali, kazi aliyoipata huenda kutokana na kisomo chake cha hali ya juu.

Ana shahada mbili za uzamili katika masuala ya uhasibu na ukaguzi wa mahesabu kutoka vyuo viwili vya haiba ya juu nchini Amerika.

Ajira hii imemsaidia kuwekeza katika nyanja mbalimbali na katika kipindi cha zaidi ya miongo miwili akihudumu katika nafasi hii, amejizolea mali kibao.

Mbali na majumba yake mawili mitaani Karen na Runda, anamiliki majumba ya watu kuishi huku wakilipa kodi katika mitaa kadhaa jijini Nairobi.

Kimaumbile, Abe pia ana mengi ya kumshukuru Mungu. Utanashati wake unaakisiwa kutoka utosini hadi miguuni, suala ambalo limemfanya kung’ang’aniwa na takriban kila binti anayekutana naye kwa mara ya kwanza.

Lakini kwa mabinti wengi, mvuto huisha pindi wanapopata fursa ya kumfahamu kwa undani.

“Kwangu, mahaba huchochewa na maumivu kwenye sehemu nyeti. Namaanisha kwamba nafurahia kupigwa na kupondwa sehemu hii kama mbinu ya kujiridhisha kimahaba. Pindi tunapoingia chumbani, bila shaka masuala ya mahaba kama vile kuvua mavazi, kupapapasana na kubusiana yatazingatiwa. Lakini ni hapo tu yatakapokomea kwani kitakachofuatia ni vita.

Vita hivi vinahusisha binti kunitandika makonde na mateke na hata kunifinya na kunikanyaga sehemu hii. Binti anapotekeleza haya sharti awe amevalia viatu vya visigino virefu.

Shughuli hii huendelea kwa muda wa saa kadhaa tukiwa mle ndani hadi nitakapolemewa kabisa na uchungu, ambapo atakuwa huru kuondoka na kuendelea na shughuli zake.

Sio kwamba nina kasoro ya kimaumbile, la, nina uwezo kama mwanamume yule mwingine. Tatizo ni kwamba sifurahishwi kamwe na tendo la ndoa. Hata nikioa, itakuwa tu kwa sababu ya kumpata mtu wa kuzungumza naye kila siku, na sio kwa sababu ya kushiriki tendo la ndoa.

Nina pesa na hivyo niko tayari kukufanyia kila kitu mradi ukubaliane nami kwamba hata tukioana, hakuna tendo la ndoa. Tamaa na uchu wetu wa kimahaba vitakuwa vikimaliziwa tu chumbani unaponipiga na kuniumiza. Hii inamaanisha kwamba hata suala la kuwa na mtoto usiliwazie. Ni suala ambalo wengi hujaribu kulikubali mwanzoni pengine kutokana na maisha ya kifahari ninayowapa.

Wengi huja wakiwa na imani ya kwamba pengine baada ya miezi kadhaa nitabadili msimamo, lakini wanapoingia na kugundua kwamba hilo halitafanyika, hutoweka ghafla”.

You can share this post!

Gavana Ottichilo atimiza ahadi ya kuwapa Vihiga Queens Sh1...

Ruto atua Nyanza akitaka Uhuru, Raila waunge mkono azma yake