Na MARGARET MAINA
Muda wa kufanya matayarisho: Dakika 15
Muda wa mapishi: Saa 1
Walaji: 5
Vinavyohitajika
Maelekezo
Osha mchele na uloweke.
Changanya nyama na chumvi na tangawizi kisha chemsha nyama kwa maji kiasi vikombe sita. Ikishaiva weka kando, na itabakia supu yake kiasi.
Weka mafuta katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vikaribie kugeuka rangi.
Tia vipande vya viazi ukaange kidogo.
Tia bizari nzima, pilipili manga, karafuu, na kijiti cha mdalasini.
Pondaponda hiliki kisha uendelee kukaanga kidogo tu.
Mimina mchele, kaanga kidogo, kisha mimina nyama na supu yake na uhakikishe unatumia maji kiasi cha vikombe tano.
Koroga kisha funika halafu upike pilau kwa moto wa wastani kiasi hadi iive.
Pakua na ufurahie.