• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 3:31 PM
KASHESHE: Sioni tena nikiwahi kuwa mke wa mtu!

KASHESHE: Sioni tena nikiwahi kuwa mke wa mtu!

Na THOMAS MATIKO

MTANGAZAJI staa wa televisheni Betty Kyalo kakata kauli kuwa katu hawezi kukubali kuwa mke nyumbani.

Betty ambaye kwa sasa anasema hana mpango wa kuolewa baada ya ndoa yake na Dennis Okari kufeli, kasisitiza kuwa maisha ya kuwa mke nyumbani ndio hawezani nayo.

Toka ndoa yake ivunjike, Kyalo kavumishwa kutokana na wanaume kadhaa akiwemo Gavana wa Mombasa Ali Hassan Joho.

“Mimi maisha ya kuwa mke nyumbani yalinishinda kabisa. Siwezi kuwa mke nyumbani niwe nakaa tu, hapana nina malengo ya kufanikisha hivyo bora ning’ang’ane kivyangu,” Betty anasema.

Kwa sasa anadaiwa kuwa kwenye mahusiano ya chini ya maji na Ali Nur almaarufu Somali bae ingawaje wawili hao wanadai kuwa ni washikaji tu.

Aidha kasisitiza kuwa licha ya kuwa na ukaribu sana na mchekeshaji Eric Omondi, katu hawezi kubali kuingia kwenye kipindi chake cha Wife Material.

Kyalo, anaiona shoo hiyo kuwa chafu mno na isiyoendana na maadili anazozizingatia yeye.

You can share this post!

KIKOLEZO: Waliambiwa ‘mtaachana tu’!

Kenya yaomba mkopo mwingine wa Sh86 bilioni kutoka Benki ya...