• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
KIKOLEZO: Maskendo kibao yachoma picha

KIKOLEZO: Maskendo kibao yachoma picha

Na THOMAS MATIKO

TUNAISHI katika nyakati za kutisha sana.

Siku hizi kuna matapeli wa kila dizaini. Wapo wanaotapeli kwa uwongo na wengine kwa jina la Mungu.

Kwenye tasnia yetu ya burudani, tuna wadau wanaotapeli mawazo ya mashabiki zao kwa jina la Mungu. Wanakesha wakihubiri maji kumbe nyuma ya pazia wenzetu wanakunywa divai.

Nafikiri katika Ukanda huu ni Kenya pekee ambapo injili inafanywa kama Showbiz. Mwaka hauwezi kuisha bila kusikia skendo kwenye tasnia ya injili. Baya zaidi ni kuwa wanaohusishwa na skendo hizi bado huendelea kujisafishia nafsi kwa kulitaja jina la Mungu utadhani ni kiumbe cha kawaida sana. Kibaya hata zaidi ni kuwa mastaa wengi wa injili kinachowayumbisha ni uhanyaji. Kweli kuna watu na viatu, kisha kuna maceleb wokovu na uasherati.

WAJESUS FAMILY

Hii ni kapo inayoundwa na Kabi pamoja na mke wake Milly. Waliamua kujiita Wajesus Family. Injili yao imekuwa ni kudhihirishia mashabiki wao kuwa ndoa hata kwa watu wachanga kama wao inawezekana kwa kumtanguliza Mungu.

Ndivyo walivyopata umaarufu. Hauwezi kupishana na posti yao hata moja isiyomtaja Yesu. Baada ya kukuza brandi yao na kuwa maarufu, sasa wameitumia kutengeneza kipato. Haina neno. Ila wiki iliyopita walichoma picha baada ya kuibuka kwa taarifa kwamba ‘watakatifu’ wamekuwa wakificha mengi ya aibu hata mbele za Mungu. Ilifichuka kwamba Kabi ana binti wa miaka saba ambaye kamtelekeza. Hii ni licha yake kuhadaa kijiji cha mashabiki wao kuwa Taj aliyezaa na mkewe Milly, ndiye mtoto wake wa pekee. Skendo hiyo ya kuwa ni ‘dead-beat’ ilipotokea, Wajesus waliamua kutengeneza vlogg kufafanua zaidi yule mtoto ni nani. Waliona fursa ya kutengeneza pesa. Kabi alimkana Abby kuwa mtoto wake na kusema kuwa ni mpwa wake kwa sababu ni mtoto wa binamu yake. Taarifa hizi zilipotoka, alijitokeza binamu yake mwingine na kutibua kuwa Kabi ndiye baba mzazi wa Abby na kuwa alimpachika ujauzito binamu yake walipokuwa kwenye mahusiano. Ameendelea kuruka stori akimkana mtoto wake peupe ila maneno ‘Praise Jesus’ ndio kaongeza dozi kutamka.

DJ MO

Madai ya tabia yake ya uasherati ndiyo yaliyosababisha yeye kupoteza kazi katika runinga ya NTV. Hii ilikuwa ni baada yake kuanikwa na binti mmoja ambaye alitoa ushahidi wa picha ya namna alivyokuwa akila uroda na DJ Mo ambaye ni mume wa mtu.

DJ Mo. Picha/ Hisani

Haikuwa mara ya kwanza kwa DJ Mo kuhusishwa na uasherati na mke wake Size 8 akamvumilia. Japo alipoteza kazi, kwa bahati nzuri hakupoteza ndoa sababu Size 8 aliamua kumsamehe tena. Hata wakati anapitia majanga haya ya kujitakia, bado aliendelea na bidii yake ya kueneza injili ya Yesu.

RINGTONE

Alianza injili vizuri ila baada ya kupata pesa na umaarufu, Ringtone aligeuka na kuwa mnyama tofauti. Amewahi kushtumiwa kwa kuwatapeli wanafunzi wa shule t-sheti zake walizolipia kipindi akiwa amehiti.

Ringtone pia kahusishwa kwenye skendo kadhaa za unyakuzi wa mali na mashamba za watu. Wiki chache zilizopita, alishtumiwa kwa madai ya kuendesha ndanguro nyumbani kwake Karen ambapo iliripotiwa amefanya tabia ya kuwaleta mademu kule kisha akawaalika marafiki zao na wote wakazini pamoja kwa kupiga ‘Sex party’. Ni madai aliyoyakana vikali huku naye jina la Mungu likiwa mdomoni.

 

DK KWENYE BEAT

Ni miaka miwili imepita toka ilipotoka ile skendo yake aliyoshtumiwa kwa kushiriki ngono na binti wa miaka 20 na kumwambukiza ugonjwa wa zinaa. Ni kitendo walichodaiwa kufanya na staa mwenzake wa injili HopeKid. Wote walipinga tena kwa jina la Mungu. Walisisitiza kwamba haikuwa kweli. Ila haikuwa mara ya kwanza kwao kutajwa kwenye skendo kama hizo. Toka skendo hiyo ilipochipuka na kupo, jamaa kama vile kabadilika. Katulia, kaoa na sasa ni baba.

BEN GITHAE

Moja kati ya hiti zake kubwa ni ile ngoma ya Ulianza na Roho. Kwenye wimbo huo Githae anaimba kwa kufuata maandiko ya Biblia. Anauliza Wakristo wenzake …mlianza na roho, mumemalizia na mwili kwa nini?…

Kwa utathmini, Githae alikuwa anatoa ushauri wa maandiko matakatifu ambayo hata yeye mwenyewe kashindwa kuyafuata. Naye miaka michache iliyopita alikiri waziwazi kwamba alienda nje ya ndoa yake kwa mke wake wa miaka mingi na hata kuishia kupata watoto. Ijapokuwa kitanda hakizai haramu, mwinjilisti Githae ana mapacha wawili waliotokana na uasherati. Hakika kanikumbusha hiti yake nyingine Tabia Mbaya. Jamaa ana tabia ya kujiimba.

You can share this post!

BI TAIFA JANUARI 29, 2021

DOMO KAYA: Tuseme kajitakia mwenyewe