• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
Atletico wamsajili Memphis Depay kutoka Barcelona ili kujaza nafasi ya Joao Felix aliyeyoyomea Chelsea

Atletico wamsajili Memphis Depay kutoka Barcelona ili kujaza nafasi ya Joao Felix aliyeyoyomea Chelsea

Na MASHIRIKA

ATLETICO Madrid wamemsajili fowadi mzoefu raia wa Uholanzi, Memphis Depay, 28, kwa Sh405 milioni kutoka Barcelona.

Depay ambaye mkataba wake na Barcelona ulitarajiwa kukatika mwishoni mwa muhula huu wa 2022-23, ametia saini kandarasi ya miaka miwili na nusu katika kikosi cha Atletico ambacho pia kinashiriki Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga).

Kwa mujibu wa makubaliano, Barcelona wako huru kujitwalia maarifa ya fowadi matata raia wa Ubelgiji, Yannick Carrasco, kutoka Atletico wakati wowote watakapojihisi.

Depay ambaye ni mchezaji wa zamani wa Manchester United, amechezea Barcelona mara nne pekee katika kampeni za msimu huu baada ya kutatizwa pakubwa na jeraha la paja.

Alihamia kambini mwa Barcelona bila ada yoyote mwanzoni mwa msimu wa 2020-21 baada ya kuagana na kikosi cha Olympique Lyon cha Ufaransa na akapachika wavuni mabao 14 kutokana na mechi 42.

Atletico walilazimika kumsajili Depay baada ya kukatiza uhusiano na fowadi Joao Felix aliyejiunga na Chelsea kwa mkopo wa msimu mmoja mwanzoni mwa Januari 2023.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Wagonjwa wakosa dawa katika hospitali ya Thika Level 5

Mung’aro afika kortini kujitetea asipoteze kiti

T L