• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 5:50 AM
Beki David Alaba ajiunga na Real Madrid bila ada yoyote

Beki David Alaba ajiunga na Real Madrid bila ada yoyote

Na MASHIRIKA

DIFENDA matata raia wa Austria, David Alaba, amejiunga rasmi na Real Madrid baada ya kuagana na Bayern Munich ya Ujerumani.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 anaingia katika sajili rasmi ya Real nchini Uhispania kwa mkataba wa miaka mitano bila ada yoyote.

Alaba alipokezwa malezi ya soka kambini mwa Bayern baada ya kujiunga na kikosi hicho mnamo 2008.

Kutua kwake kambini mwa Real kunatokea siku chache baada ya kocha raia wa Ufaransa, Zinedine Zidane kujiuzulu baada ya miamba hao wa Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) na Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kukamilisha kampeni za msimu wa 2020-21 bila taji lolote.

Ni mara ya kwanza tangu 2009-10 kwa Real kukamilisha kampeni za msimu bila kujizolea kombe.

Alaba aliwajibishwa na Bayern katika jumla ya michuano 431 katika kipindi cha miaka 13 uwanjani Allianz Arena.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Yabainika De Bruyne aliumia jicho na kuvunjika pua wakati...

Uhuru aangusha minofu kwa Raila