• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Benzema afunga mabao mawili na kupaisha Real Madrid hadi nafasi ya pili kwenye La Liga

Benzema afunga mabao mawili na kupaisha Real Madrid hadi nafasi ya pili kwenye La Liga

Na MASHIRIKA

KARIM Benzema alifunga mabao mawili na kusaidia Real Madrid kuweka kando maruerue ya kubanduliwa mapema kwenye Spanish Cup kwa kuwakomoa Alaves 4-1 katika Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga).

Real waliduwazwa na Alcoyano ya Ligi ya Daraja la Tatu nchini Uhispania iliyowadengua kwenye gozi la kuwania taji la Copa del Rey msimu huu mnamo Januari 20, 2021.

Mabingwa hao watetezi wa La Liga walichukuwa uongozi kupitia Casemiro katika 15 kabla ya Benzema na Eden Hazard kufanya mambo kuwa 3-0 kufikia mwisho wa kipindi cha kwanza.

Ingawa Joselu Luis Mato alipania kuwarejesha Alaves mchezoni katika dakika ya 59, chombo chao kilizamishwa na Benzema kunako dakika ya 70.

Ushindi huo wa Real uliwapaisha hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa jedwali la La Liga kwa alama 40, saba nyuma ya viongozi Atletico Madrid ambao wana mchuano mmoja zaidi wa kutandaza ili kufikia idadi ya mechi ambazo zimesakatwa na washindano wao wakuu – Real, Barcelona na Sevilla.

Kocha Zinedine Zidane hakusimamia mchuano huo kati ya Real na Alaves kwa kuwa anaugua Covid-19.

You can share this post!

DIMBA: ‘Big Mo’ Kean ametajwa kama kizazi kipya...

Seneta Mwaura aitaka serikali ijenge madarasa zaidi shule...