• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 9:50 AM
KCB yapiga jeki gofu ya Safari Tour kwa Sh1 milioni

KCB yapiga jeki gofu ya Safari Tour kwa Sh1 milioni

Na GEOFFREY ANENE

BENKI ya KCB imetangaza kudhamini raundi ya mwisho ya mashindano ya gofu ya Safari Tour kwa Sh1 milioni, Ijumaa.

Mashindano hayo yatafanyika katika klabu ya gofu ya Muthaiga mjini Nairobi mnamo Februari 11-15. Akizungumza katika hafla ya kutoa hundi jijini Nairobi, Mkurugenzi wa Mauzo na Mawasiliano Rosalind Gichuru amesema kuwa udhamini huo ni ithibati ya benki hiyo kujitolea katika kukuza michezo nchini Kenya.

“KCB si mgeni katika shughuli za kusaidia michezo humu nchini. Tumesaidia fani mbalimbali kifedha zikiwemo riadha, soka, gofu na raga kwa miaka mingi,” amesema.

Gichuru ameongeza, “Raundi ya mwisho ya Safari Tour ya msimu 2022-2023 inatupatia fursa muhimu ya kusaidia wachezaji wetu wa hapa nyumbani kujiandaa kwa mashindano ya Magical Kenya Open yatakayofanyika baadaye mwezi Machi. Sh1 milioni tunazotoa kupiga jeki raundi ya mwisho ni zawadi.”

Baada ya raundi ya Muthaiga, majina ya Wakenya watakaoshiriki Magical Kenya Open hapo Machi 9-12, yatatangazwa.

Benki ya KCB ilidhamini mashindano ya wanawake ya Magical Kenya Open yaliyokamilika katika klabu ya Vipingo kaunti ya Kilifi wikendi iliyopita.

  • Tags

You can share this post!

Warembo wa Lyon wapewa Chelsea huku Arsenal wakimenyana na...

Kidosho azua gumzo Facebook kwa kumtambalia mtangazaji...

T L