Na MASHIRIKA
VIPUSA wa Chelsea watakutana na Olympique Lyon ambao ni mabingwa watetezi wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kwenye robo-fainali ya kipute hicho msimu huu wa 2022-23.
Arsenal watavaana na Bayern Munich ya Ujerumani huku Barcelona walioambulia nafasi ya pili kwenye UEFA mnamo 2021-22, wakikutanishwa na limbukeni AS Roma ya Italia. Malkia mara nane wa kivumbi hicho watachuana na Wolfsburg kutoka Ujerumani.
Mechi za mkondo wa kwanza wa robo-fainali zitasakatwa kati ya Machi 21 na 22 huku michuano ya marudiano ikipigwa wiki moja baadaye.
Chelsea waliodenguliwa kwenye UEFA katika hatua ya makundi mwaka jana, walitia fora zaidi muhula huu huku wakijizolea alama 16 kutokana na mechi sita.
Arsenal, waliong’olewa na Wolfsburg kwenye robo-fainali msimu uliopita, watavaana na Bayern ambao pia walibanduliwa na PSG katika hatua hiyo ya nane-bora.
Georgia Stanway, ambaye ni mshindi wa taji la UEFA, atakabiliana na kikosi cha Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake nchini Uingereza (WSL) kwa mara ya kwanza tangu aagane na Manchester City na kuyoyomea kambini mwa Bayern mnamo 2022.
Bayern Munich vs Arsenal
Lyon vs Chelsea
AS Roma vs Barcelona
PSG vs Wolfsburg
PSG/Wolfsburg vs Bayern/Arsenal
Chelsea/Lyon vs Barcelona/Roma
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO