• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 12:11 PM
Warembo wa Lyon wapewa Chelsea huku Arsenal wakimenyana na Bayern Munich kwenye robo-fainali za UEFA

Warembo wa Lyon wapewa Chelsea huku Arsenal wakimenyana na Bayern Munich kwenye robo-fainali za UEFA

Na MASHIRIKA

VIPUSA wa Chelsea watakutana na Olympique Lyon ambao ni mabingwa watetezi wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kwenye robo-fainali ya kipute hicho msimu huu wa 2022-23.

Arsenal watavaana na Bayern Munich ya Ujerumani huku Barcelona walioambulia nafasi ya pili kwenye UEFA mnamo 2021-22, wakikutanishwa na limbukeni AS Roma ya Italia. Malkia mara nane wa kivumbi hicho watachuana na Wolfsburg kutoka Ujerumani.

Mechi za mkondo wa kwanza wa robo-fainali zitasakatwa kati ya Machi 21 na 22 huku michuano ya marudiano ikipigwa wiki moja baadaye.

Chelsea waliodenguliwa kwenye UEFA katika hatua ya makundi mwaka jana, walitia fora zaidi muhula huu huku wakijizolea alama 16 kutokana na mechi sita.

Arsenal, waliong’olewa na Wolfsburg kwenye robo-fainali msimu uliopita, watavaana na Bayern ambao pia walibanduliwa na PSG katika hatua hiyo ya nane-bora.

Georgia Stanway, ambaye ni mshindi wa taji la UEFA, atakabiliana na kikosi cha Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake nchini Uingereza (WSL) kwa mara ya kwanza tangu aagane na Manchester City na kuyoyomea kambini mwa Bayern mnamo 2022.

DROO YA ROBO-FAINALI YA UEFA:

Bayern Munich vs Arsenal

Lyon vs Chelsea

AS Roma vs Barcelona

PSG vs Wolfsburg

DROO YA NUSU-FAINALI YA UEFA:

PSG/Wolfsburg vs Bayern/Arsenal

Chelsea/Lyon vs Barcelona/Roma

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

‘Waititu hafai kusafisha mito jijini Nairobi’

KCB yapiga jeki gofu ya Safari Tour kwa Sh1 milioni

T L