Na MASHIRIKA
BRIGHTON wamemsajili kipa chipukizi raia wa Uholanzi, Kjell Scherpen kutoka klabu ya Ajax.
Mlinda-lango huyo mwenye umri wa miaka 21 aliwajibishwa mara nne katika kikosi cha kwanza cha Ajax baada ya kusajiliwa kutoka FC Emmen mnamo Julai 2019.
Hadi alipojiengua kambini mwa Ajax, Scherpen ambaye ni tegemeo kubwa katika kikosi cha Uholanzi cha chipukizi wasiozidi umri wa miaka 21, alikuwa amesalia na miaka miwili katika mkataba wake na klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Eredivisie. Scherpen ana urefu wa futi sita na inchi nane.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO