• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:35 AM
Man-United wapewa Forest huku Southampton wakikutana na Newcastle kwenye nusu-fainali ya Carabao Cup

Man-United wapewa Forest huku Southampton wakikutana na Newcastle kwenye nusu-fainali ya Carabao Cup

Na MASHIRIKA

MANCHESTER United watavaana na Nottingham Forest nao Southampton kumenyana na Newcastle United kwenye nusu-fainali ya Carabao Cup muhula huu wa 2022-23.

Chini ya kocha Steve Cooper, Forest watakuwa wenyeji wa mchuano wa mkondo wa kwanza dhidi ya Man-United baada ya kudengua Wolverhampton Wanderers kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya 1-1 mnamo Jumatano.

Licha ya kuvuta mkia wa jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL), Southampton walidengua Manchester City kwa kichapo cha 2-0 mnamo Jumatano usiku ugani St Mary’s ma kutinga nusu-fainali ya Carabao Cup.

Mechi za mikondo miwili ya nusu-fainali imeratibiwa kutandazwa katika wiki zinazoanda Januari 23 na 30, 2023.

Man-United walijikatia tiketi ya kunogesha nusu-fainali ya Carabao Cuo muhula huu baada ya kupokeza Charlton ya Ligi ya Daraja ya Pili nchini Uingereza (League One) kichapo cha 3-0 mnamo Jumanne usiku ugani Old Trafford.

Man-United wanajivunia kunyanyua taji la Carabao Cup mara tano katika historia, mara ya mwisho kabisa ikiwa mwaka wa 2017. Waliwahi kupepeta Forest kwenye fainali ya kipute hicho mnamo 1992.

Newcastle wanaokamata nafasi ya tatu kwenye msimamo wa jedwali la EPL, waliingia hatua ya nne-bora ya Carabao Cup baada ya kutandika Leicester 2-0.

DROO YA NUSU-FAINALI YA CARABAO CUP:

Nottingham vs Man-United

Southampton vs Newcastle

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

MAWAIDHA YA KIISLAMU: Malezi bora ya watoto yahitajika...

DRC yakemea Rwanda kuwakataa wakimbizi

T L