Na MASHIRIKA
KAKA wawili raia wa Uingereza – Ken na Neal Skupski waliwabwaga Marcel Granollers na Horacio Zeballos na kutwaa taji la tenisi la Mexican Open kwa wachezaji wawili wawili jijini Acapulco.
Ndugu hao walishinda kwa seti tatu za 7-6, 7-3 na 6-4.
Ushindi huo ulikuwa wao wa tatu pamoja na wa kwanza tangu 2019, baada ya kutengana kwa muda kabla ya kurudiana mwanzoni mwa msimu huu.
“Muda umekuwa mrefu na safari imekuwa ngumu tangu tulipotengana kisha kurudiana. Ushindi huu ni muhimu sana katika kutuunganisha hata zaidi,” akasema Ken Skupski.
Katika kitengo cha mchezaji mmoja mmoja, Alexander Zverev alimpiku Stefanos Tsitsipas kwa seti tatu za 6-4, 7-6 na 7-3 na kutia kibindoni taji lake la 14 la mashindano ya ATP Tour.
Zverev ambaye ni raia wa Ujerumani, alijinyanyua baada ya kujipata chini kwa alama 4-1 kwenye seti ya kwanza.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO