• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 7:47 PM
Pigo Barcelona jeraha likitarajiwa kumweka nje Aguero kwa wiki 10

Pigo Barcelona jeraha likitarajiwa kumweka nje Aguero kwa wiki 10

Na MASHIRIKA

MSHAMBULIAJI matata wa Barcelona, Sergio Aguero, atasalia nje kwa wiki 10 kuuguza jeraha la mshipa wa mguu wake wa kulia.

Aguero, 33, alijiunga na Barcelona kutoka Manchester City kwa mkataba wa miaka miwili mnamo Juni 2021.

Alihudumu kambini mwa Man-City kwa kipindi cha miaka 10 na akawa mfungaji bora wa muda wote kambini mwa kikosi hicho baada ya kupachika wavuni mabao 260 kutokana na mechi 390.

Aguero alikuwa sehemu ya kikosi kilichoshindia Argentina ubingwa wa taji la Copa America mwaka huu wa 2021.

Fowadi mwenzake kambini mwa Argentina, Lionel Messi tayari amethibitisha kuagana na Barcelona na amekubaliana na PSG kumsajili kwa kandarasi ya miaka miwili.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Jumwa ashindwa kushawishi mahakama iahirishe kesi yake ya...

Makundi 10 ya wafanyabiashara Thika yapokea mkopo wa Sh1.4...