• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 1:14 PM
RB Leipzig wamsajili beki Angelino kutoka Manchester City

RB Leipzig wamsajili beki Angelino kutoka Manchester City

Na MASHIRIKA

KLABU ya RB Leipzig imemsajili beki matata raia wa Uhispania, Angelino Esmoris Tasende, 24, kwa mkataba wa kudumu kutoka Manchester City hadi mwishoni mwa mwaka 2025.

Angelino alirejea kambini mwa Leipzig kwa kipindi cha pili cha mkopo mnamo Septemba 2020 na kikosi hicho cha Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) kimemtwaa sasa kabisa.

Tangu aingie kambini mwa Leipzig, beki huyo amechangia mabao 16 kutokana na mechi 47 ambazo amezisakata.

Hadi alipoondoka uwanjani Etihad, Uingerea, alikuwa amechezea Man-City waliomsajili kutoka PSV Eindhoven ya Uholanzi mnamo 2018 mara 15

“Angelino ni mchezaji wa haiba kubwa ambaye atachangia kuweka hai matumaini yetu ya kuwania mataji kadhaa katika kampeni za msimu huu,” akasema kocha wa Leipzig, Julian Nagelsmann.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Bayern Munich wajinasia maarifa ya Upamecano baada ya...

Shujaa na Lionesses kuelekea Uhispania usiku wa kuamkia...