Na MASHIRIKA
TOTTENHAM Hotspur wanawania maarifa ya fowadi Lautaro Martinez wa Inter Milan na wako radhi kuweka mezani Sh9.3 bilioni ili kumsajili.
Martinez, 23, amefungia Inter mabao 49 kutokana na mechi 132 tangu abanduke kambini mwa Racing Club ya Argentina mnamo 2018. Alikuwa sehemu muhimu ya kikosi kilichoshindia Inter ubingwa wa Ligi Kuu ya Italia (Serie A) mnamo 2020-21 na akasaidia Argentina pia kuzoa taji la Copa Amerika mnamo Julai 2021.
Kufikia sasa, Spurs wametumia zaidi ya Sh9.3 bilioni kujisuka upya baada ya kumsajili beki Cristian Romero kutoka Atalanta ya Italia kwa Sh6.6 bilioni wiki iliyopita.
Fowadi Bryan Gil aliyetokea Sevilla ya Uhispania na Pierluigi Gollini aliyeagana na Atalanta ndio sajili wengine wapya wa Spurs ambao sasa wanatiwa makali na kocha Nuno Espirito Santo.
Kufaulu kwa mpango wa Martinez kutua Spurs kutachochea kikosi hicho cha Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kuagana na Harry Kane anayehemewa pakubwa na Manchester City.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO