• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 1:14 PM
Suarez afunga mabao mawili na kusaidia Atletico Madrid kutua kileleni mwa jedwali la La Liga

Suarez afunga mabao mawili na kusaidia Atletico Madrid kutua kileleni mwa jedwali la La Liga

Na MASHIRIKA

LUIS Suarez alifunga mabao mawili mwishoni mwa kipindi cha pili na kusaidia waajiri wake Atletico Madrid ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) kutoka nyuma na kusajili ushindi wa 2-1 dhidi ya Getafe.

Bao la kwanza la Getafe dhidi ya Atletico tangu 2011 lilifumwa wavuni baada ya mpira wa kichwa uliopigwa na Stefan Mitrovic kugonga mhimili wa lango la Getafe na kumbabatiza kipa Jan Oblak.

Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa Getafe kufunga Atletico baada ya mechi 20 tangu kocha Diego Simeone aaminiwe fursa ya kudhibiti mikoba ya Atletico.

Kuondolewa kwa Carles Alena uwanjani baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu kuliwapa Atletico nafasi ya kuwateremkia wenyeji wao na Suarez akapachika wavuni magoli mawili na kuendeleza rekodi ya kutopigwa kwa Atletico hadi kufikia sasa ligini msimu huu.

Mabao ya Suarez yalikuwa zao la ushirikiano mkubwa kati yake na wanasoka Mario Hermoso na Sime Vrsaljko. Hadi alipopangwa katika kikosi cha kwanza cha Atletico dhidi ya Getafe, Suarez alikuwa amefungia waajiri wake bao moja pekee kutokana na mechi sita.

Atletico kwa sasa wanaselelea kileleni mwa jedwali la La Liga kwa alama 14, moja zaidi kuliko Real ambao wana mchuano mmoja zaidi wa kusakata ili kufikia idadi ya mechi ambazo zimetandazwa na Real ya kocha Carlo Ancelotti.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Bei ya juu ya gesi yasukuma Wakenya kukumbatia makaa, kuni

CBC: Kuppet pia wana malalamishi